Saturday, September 3, 2016

UTAWALA BORA 1

SEHEMU YA KWANZA

UTAWALA BORA

Utawala ni matumizi ya mamlaka ya kisiasa, kiuchumi au
vinginevyo katika kusimamia masuala ya nchi kwenye ngazi
zote.
Utawala bora ni matumizi ya mamlaka ambayo yanakuwa na
uwazi, uwajibikaji, ushirikishaji wa watu, ufanisi, tija, uadilifu
usawa na unafuata utawala wa sheria.

Ili kutekeleza dhana ya utawala bora mambo yafuatayo lazima
yazingatiwe:
• Matumizi sahihi ya dola,
• Matumizi mazuri ya rasilimali kwa faida ya wananchi,
• Matumizi mazuri ya madaraka yao,
• Kujua na kutambua madaraka waliyonayo na matumizi
yake,
• Madaraka yanatumika kulingana na mipaka iliyowekwa na
katiba na sheria.
Utawala ni matumizi ya mamlaka ya kisiasa, kiuchumi au
vinginevyo katika kusimamia masuala ya nchi kwenye ngazi
zote.
Utawala bora ni matumizi ya mamlaka ambayo yanakuwa na
uwazi, uwajibikaji, ushirikishaji wa watu, ufanisi, tija, uadilifu
usawa na unafuata utawala wa sheria.

Ili kutekeleza dhana ya utawala bora mambo yafuatayo lazima
yazingatiwe:
• Matumizi sahihi ya dola,
• Matumizi mazuri ya rasilimali kwa faida ya wananchi,
• Matumizi mazuri ya madaraka yao,
• Kujua na kutambua madaraka waliyonayo na matumizi
yake,
• Madaraka yanatumika kulingana na mipaka iliyowekwa na
katiba na sheria.

Faida za Utawala Bora

Utawala bora unasaidia kuwa na mambo yafuatayo:
• Matumizi mazuri ya rasilimali za nchi,
• Maendeleo endelevu,
• Kupungua kwa umasikini, ujinga na maradhi,
• Kutokomea kwa rushwa,
• Huduma bora za jamii,
• Amani na utulivu,
• Kuheshimiwa kwa haki za binadamu,
• Utatuzi wa migogoro kwa mujibu wa sheria na taratibu,
• Kuleta ustawi wa wananchi.

No comments:

Post a Comment