Saturday, September 3, 2016

HAKI ZA BINADAMU

HAKI ZA BINADAMU

Haki za binadamu ni stahili alizonazo kila binadamu kwa asili
ya kuwa binadamu.
Vyanzo vya Haki za Binadamu nchini Tanzania
Chanzo kikuu cha haki za binadamu nchini Tanzania ni Katiba ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977. Sambamba
na Katiba, vipo vyanzo vingine vya haki za binadamu nchini,
kama vile, Sheria ya Mtoto Namba 21 ya mwaka 2009, Sheria
ya Watu Wenye Ulemavu Namba 9 ya mwaka 2010, Sheria ya
Kuzuia na Kudhibiti Ukimwi Namba 28 ya mwaka 2008, Sheria
ya Ajira na Mahusiano Kazini namba 6 ya mwaka 2004, Sheria
ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, Sura ya 20 (R.E. 2002) na
mikataba mbalimbali ya haki za binadamu ya kimataifa na ya
kikanda ambayo Tanzania imeisaini na kuiridhia.

No comments:

Post a Comment