Saturday, September 3, 2016

ELimu Y Uraia kupelekwa Bungeni.

                                                   ELimu Y Uraia kupelekwa Bungeni
.

Makamu wa Rais SAMIA SULUHU HASSAN ameiomba Taasisi ya HANNS SEIDEL FOUNDATION isaidie kupeleka elimu ya uraia katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa TANZANIA ili Wabunge wa bunge hilo waweze kujua wajibu wao ndani na nje ya bunge.
SAMIA ametoa ombi hilo Ikulu Jijini DSM alipokutana na ujumbe wa Taasisi hiyo uliomtembelea ofisi kwake kwa lengo la kutaka kujua kama ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa TANZANIA kuna sheria na kanuni za kuendesha vikao vya Bunge.

Makamu wa Rais Ameueleza ujumbe huo ulioongozwa na Mwenyekiti wa Hanns Seidel Foundation Profesa URSULA MANNK kuwa sheria na kanuni zipo za kuendesha vikao vya Bunge lakini baadhi ya wabunge hawazifuati kama inavyotakiwa.

Tasisi ya Hanns Seidel Foundation yenye makao yake makuu yake Mjini MUNICH nchini UJERUMANI inajishughulisha na masuala ya demokrasia, amani na maendeleo na inaendesha shughuli zake katika nchi zaidi ya 60 duniani.
August 11, 2016
TBC-Taarifa

No comments:

Post a Comment